Ujumbe, 25 Septemba 2024
“Wanangu wapendwa! Kwa kuwapenda ninyi, Mungu alinituma kati yenu ili kuwapenda ninyi na kuwasihi katika sala na uongofu, kwa ajili ya amani ndani yenu, katika familia zenu na katika dunia. Wanangu, msisahau kwamba amani ya kweli huja tu, kwa njia ya maombi, kutoka kwa Mungu ambaye ndiye amani yenu. Asanteni kwa kuitikia wito wangu. ”