Ujumbe, 25 Juni 2025
“Wanangu wapendwa! Pia leo namshukuru Mwenyezi kwa kuwa pamoja nanyi na kuweza kuwaongoza kuelekea kwa Mungu wa upendo na amani. Itikadi zinazowabomoa ninyi na maisha yenu ya kiroho ni za mpito. Ninawaita ninyi wanangu, mrudieni Mungu kwa maana kwa Mungu mnayo wakati ujao na uzima wa milele. Asanteni kwa kuitikia wito wangu. ”